Mbunge wa Embakasi Mashariki Paul Ongili alias Babu Owino Jumapili, Novemba 3, alituma picha yake akipata matibabu hospitalini.
Mbunge huyu amekuwa akiugua kwa muda wa wiki moja iliyopita na alikuwa hospitalini juu ya ugonjwa ambao haujulikani.
Alishiriki picha akiwa amelazwa katika kitengo cha radiology akisubiri matibabu.
“Mungu aniponye kwa sababu lazima niongoze taifa hili siku moja,” alisema kupitia Facebook yake.
Haijabainika wazi ni lini mbunge huyo alianza kuugua lakini upekuzi wetu unaonyesha amekuwa nje ya uwezo kwa sababu hiyo hiyo, akakosa kampeni muhimu za Kibra kwa mgombea wa ODM Benard ‘Imran’ Okoth.
Babu ambaye alizungumza na Wakenya.co.ke siku ya Alhamisi, Oktoba 31 alifunguka kuwa alikuwa hospitalini akipokea matibabu akishindwa kutaja kile alikuwa akiugua.