Mke wa marehemu Ken Okoth, Monica Lavender Okoth, ametupilia mbali matokeo ya DNA kuonyesha kuwa mumewe alizaa mtoto na mwakilishi wa wadi aliyeteuliwa Anne Thumbi.
Siku ya Jumatano, Septemba 18, mama wa Okoth, Angeline Ajwang, Monica, na Bi Thumbi walikuwa wamerudi kortini kutoa maoni rasmi ikiwa kila mmoja wao amekubali au alikataa matokeo ya DNA ya Septemba 5.
Angeline alithibitisha kuwa amekubali matokeo ya uchunguzi wa DNA na akauliza korti iondoe kesi ya Thumbi kutaka kujua baba wa mtoto wake.
Monica, kwa upande mwingine, hakuridhika na matokeo ya uchunguzi. Aliiambia korti kuwa alikuwa ameamuru vipimo vya DNA vya kujitegemea kwa mwana wa Okoth na Thumbi, na bado hakupata matokeo.
Kwa hivyo, Monica aliiuliza mahakama kumruhusu atoe siku 20 kupata matokeo, lakini hakimu aliagiza apewe siku 15 ili kudhibitisha ikiwa vipimo vilivyotumwa naye vitatoa matokeo tofauti.
Matokeo ya DNA yaliyowasilishwa na mawakili wa Thumbi wiki mbili zilizopita yalithibitisha kuwa kweli Ken alikuwa baba wa mtoto wake.
Katika matokeo yaliyowasilishwa na wakili Danstan Omari anayewakilisha mama wa mtoto, matokeo ya DNA yalirudisha uamuzi wa asilimia 99.99.
LATE Ken Okoth's wife Monica disputes DNA results presented by Ann Thumbi's lawyers. pic.twitter.com/3sdNKzZo0J
— The Star Breaking (@TheStarBreaking) September 18, 2019
Vipimo vitatu vya DNA yaliyofanywa ndani na nje ya nchi yalionyesha matokeo sawa.
Korti ya hakimu iliagiza uchunguzi wa DNA ufanyike baada ya mtoto na mama yake kutengwa kwa kuwa sehemu ya mchakato wa mazishi ya Ken Okoth.
Ndugu wengine wa marehemu Okoth walikuwa wamekataa kuwakubali kama sehemu ya familia.
“Mbunge marehemu Okoth ndiye baba wa mtoto mdogo, ambaye ndiye alikuwa maudhui wa mzozo. Tumewasilisha matokeo ya DNA ya ndani kama ishara ya kujiamini kwa vituo vya matibabu vya Kenya, “wakili Omari alisema.
Alisisitiza kwamba watatoa matokeo yale yale kwa wanafamilia wengine wa marehemu ambao walikuwa wakitilia shaka kuwa yeye ni baba wa mtoto.