Chansela wa chuo kikuu cha Maasai Mara ajibu ufichuzi wa wizi

Image
Profesa Mary Walingo Chansela chuo kikuu cha Maasai Mara Picha: Kwa Hisani

Chansela wa Chuo Kikuu cha Maasai Mara Profesa Mary Walingo hatimaye amejibu ufichuzi wa uwizi mkubwa katika Taasisi hiyo.

Walingo ambaye alielezwa kama ‘Ng’ombe kubwa’ katika uchunguzi wa runinga ya Citizen iliyoitwa ‘Mara Heist’, siku ya Jumapili alikanusha madai wa kuwa katikati mwa ufisadi wa chuo hicho.

Badala yake, Walingo anatoa sifa kwa Citizen TV akidai kuwa amekuwa akipigania kwa muda mrefu kuwachana watu wanyonge ambao huiba hatma ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Maasai Mara.

“Ningependa kuchukua nafasi hii kuwashukuru Citizen TV kwa kuangazia wizi ambao umekithiri katika Chuo Kikuu cha Maasai Mara. Inanisaidia katika uchunguzi ambayo nimekuwa niking’ang’ana nayo kwa muda sasa. Uporaji huu usiofaa wa wizi sio tu kuiba hatma ya watoto wetu lakini pia huathiri ukuaji wa taasisi yetu, “alisema.

Walingo anaendelea kudai kwamba mtu yeyote aliyehusika na tukio la Mara Heist anapaswa kuwa tayari kukabiliana na sheria kamili.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *