Jimmy Gait Afichua Matokeo ya matibabu Pamoja na Hofu ya Saratani [VIDEO]

Image result for jimmy gait

Mwimbaji wa nyimbo za Injili, Jimmy Gait, Jumanne jioni, alitangaza matokeo aliyoyachukua wakati wa matibabu nchini India, na alionyesha mshtuko wake.

Akihutubia mashabiki wake kupitia video kwenye YouTube, mwanamuziki huyo alifichua kwamba alishangazwa na matokeo aliyoyapata kutoka kwa madaktari wa India, ambayo yalipingana na ambayo mwenzake wa Kenya alikuwa amempatia.

Gait alielezea kuwa madaktari wa Kenya walikuwa wamependekeza kwamba afanyiwe upasuaji wa koo, hata bila kumfanyia uchunguzi.

Huko India, hata hivyo, daktari aliendesha vipimo kadhaa ili kujua chanzo cha shida ni nini na kuwa operesheni haikuwa lazima. Alikuwa akiugua wingi wa aisidi kwa mwili.

Image result for jimmy gait

vipimo pia vilionyesha kuwa shida ilitoka kwa tumbo na kwamba ikiwa ingeachwa bila kutibiwa, ingepelekea kuwa na saratani.

“Jambo la kushangaza ni kwamba madaktari wa Kenya walinipatia mapendekezo mabaya na kama wangenifanyia upasuaji, shida isingekuwa imetatuliwa kwa sababu ilikuwa inatoka kwenye tumbo langu,” alielezea Jimmy Gait.

Alishutumu zaidi madaktari wa Kenya kwa kuwa na tamaa, kwani walikuwa tayari kufanya operesheni mradi tu angetoa noti nono.

Tazama video kamili;

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *