Sonko achemka baada ya maswali magumu kwenye mahojiano ya televisheni

Gavana Sonko na mtangazaji Anne Kiguta Picha: Kwa Hisani

Gavana wa Nairobi, Mike Sonko, Jumapili usiku, alichemka baada ya mtangazaji wa K24 TV, Anne Kiguta kumuuliza maswali za kibinafsi wakati wa mahojiano.

Mtangazaji huyo shupavu alirejelea suala la Sonko la hivi karibuni ambapo alijibizana kwa maneno makali na Mwakilishi wake wa wanawake, Esther Passaris, na mbunge wa Suba Kaskazini, Millie Odhiambo.

Kiguta alisisitiza tukio ambalo Sonko alimshambulia Passaris mbele ya umati wa watu akidai kuwa hakuwa na mwelekeo wa kupokea simu zake kwa kuwa yeye sio mume wake.

Nairobi Woman Rep Esther Passaris with Nairobi County Commisioner Flora Mworoa and Governor Mike Sonko at Pumwani Police Grounds on 1/6/2019
Gavana Sonko, Rais Uhuru Kenyatta na Esther Passaris Picha: Kwa Hisani

Hapo awali alikuwa amechapisha kwenye mtandao wa Facebook akilaani afya ya uzazi ya Millie baada ya kumshtumu kwa kuanzisha shambulio dhidi yake.

Kama kwamba hajafurahishwa na maoni yake, gavana alimkumbusha mtangazaji kuwa alikuwa anaenda mbali sana na kwamba alikuwa akiuliza maswali yasiyofaa.

Alifikia wakati ambapo alimwambia Kiguta kwamba yeye sio mume wake kama tu alivyofanya kwa Passaris.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *