Naibu mwenyekiti wa zamani wa AFC Leopards afariki kwa ajali

Left: Felix Shitsama, Right: accident wreckage

Naibu wa zamani wa AFC Leopards Felix Shitsama ameaga dunia.

Shitsama ambaye alikuwa na marafiki wawili alikufa katika ajali mbaya ya barabara iliyotokea katika eneo la Timboroa Jumamosi.

Walikuwa wakielekea Malava kwa mazishi ya familia kabla ya janga hilo kutokea.

Image result for shitsama

Wakithibitisha tukio hilo, AFC Leopards kupitia ukurasa yao rasmi ya Facebook ilisema kwamba Shitsama ambaye alikuwa kwenye kiti cha dereva alikufa wakati wengine wawili walikuwa na majeraha madogo.

Wawili hao walikimbizwa hospitalini huko Eldoret. Ripoti zinasema kuwa wamepata matibabu na kuondoka hospitalini.

Marehemu Shitsama alichaguliwa mnamo 2016 kuwa makamu wa kilabu hicho katika Kituo cha Michezo cha Kimataifa cha Moi Kasarani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *