Waliosema kuwa mtandao hauwezi kusahau hawakukosea kwani siku ya Jumatano, baadhi ya Wakenya walimdihaki naibu rais William Ruto.
Nyuma mnamo 2017, wakati akiwa kwenye harakati za kampeni, naibu rais William Ruto alikuwa ameahidi kurejesha uwanja wa kihistoria wa Kimariny, West Pokot, katika kipindi cha chini ya miezi 6.
“Katika muda wa miezi sita, uwanja huko Kimariny huko West Pokot, ambao ni wa kihistoria utakuwa kamili, “alisisitiza.
Video ya ahadi yake kwa watu wa West Pokot iliibuka tena, na Wakenya walimwambia wazi Ruto kuwa ni mdanganyifu.
Uwanja wa Kimariny ulijulikana kwa kukuza wanariadha waliovunja rekodi, ambao waliendelea kushinda ulimwengu wakati wakirusha bendera ya kitaifa ya Kenya.
Walakini, licha ya ahadi hiyo, kazi za ukarabati zilisikika mara tu zinaanza, na gazeti la Daily Nation likiripoti kwamba uwanja huo kwa sasa unafanana na shamba lililotelekezwa.
"In six months time, the stadium in Kamariny in West Pokot, which is historic will be complete" DP Ruto in 2013.
Kamariny Stadium remains incomplete in 2019. https://t.co/4BnQudOc8Y pic.twitter.com/y1Gz4suzT6
— Augustine Sang 🇰🇪 (@Sang_254) August 14, 2019