Wendy Waeni ambaye ni mwanasarakasi tajika ameshtua taifa baada ya kufichua meneja wake wa zamani Joe Mwangi kama mtu tapeli.
Wendy aliibuka miaka michache iliyopita na amejulikana kwa kufanya sarakasi na kuigiza kwa wakuu wa nchi kadha wa kadha.
Hivi karibuni alipata nafasi akiwa na Joe Mwangi, kuigiza kwa rais Kenyatta, mwenzake Kagame, na hata akasafiri kwenda China na sehemu zingine za ulimwengu.
Walakini, Wendy Waeni tunayemwona kwenye mitandao ya kijamii sio Wendy halisi, meneja wake wa zamani Joe Mwangi amekuwa akiposti picha zake Waeni na hata kutoa maoni yake kwenye mitando.
Mwaka wa 2017, kupitia ukurasa wa Waeni wa Instagram, video iliwekwa mwanaarakasi huyo akilindesha na kufurahia ‘Range Rover Velar mpya’ ambayo wafuasi wake walisifia kuwa kwa kweli, ‘Amefika’.
Ladies and Gentlemen, i bring to you Joe mwangi a great scammer after the fixed match sellers. Man has misused wendys chance by misusing all her earnings. Her mum is a hawker in town, whereas Wendy is out there smashing the cash 😪.https://t.co/NrW6ciViEh pic.twitter.com/6KOxxbCJxq
— Kikuyu blogger (@itsmwangih) August 8, 2019
Wakenya kwenye Twitter walishtushwa na ufunuo wa Wendy ambao wameona kwamba Joe Mwangi amekuwa akimtumia vibaya ili kujinufaisha mwenyewe.
Wendy Waeni is a child & I trust her word … Joe Mwangi used her & her social media accounts to enrich himself … Joe exploited her innocence to get access to Presidents & powerful men … Joe Mwangi should be charged with international crimes of Child Slavery & Trafficking.
— Donald B Kipkorir (@DonaldBKipkorir) August 8, 2019
How can this man Joe Mwangi frustrate Wendy and her single mum?? Some people just scoop too many curses with a spade literally 🤦
— Sylvia Ndunge (@Syshndunge) August 8, 2019