Mahakama yafanya maamuzi ya kwanza kwenye kesi iliyowasilishwa na makampuni ya kamari

Image result for betting firms in kenya

Mambo yanaendelea kuenda segemnege kwa makampuni zinazoendesha biashara ya michezo za kamari. Hii ni baada ya korti kutupilia mbali mswada wao dhidi ya tume ya udhiti wa michezo za bahati nasibu (BCLB).

Advanced Gaming Limited, ambayo ni moja kati ya makampuni, ilikuwa imeomba korti kuizimamisha amri la BCLB wa kuisimamisha kampuni hiyo wiki jana.

Makampuni yaliafikiana kungoja hadi kesi dhidi yao isikizwe kwenye mahakama kuhusu kufungwa kwa biashara zao.

Image result for betting firms in kenya

Jaji Weldon Korir, hata hivyo, alikataa kutoa amri za kihafidhina akisema kwamba hakuona haja.

Kesi hiyo imehairishwa hadi tarehe 26 mwezi huu wa Julai.

Makampuni 27 kwa sasa yamefungwa na mfumo wa malipo wa Paybill kuvunjiliwa mbali huku wakurugenzi 17 ambao ni wageni wakiamrishwa kuhamishwa kutoka Kenya kwa mujibu wa Waziri wa ndani Fred Matang’i.

 

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *