Hayawi hayawi mwishowe huwa, baada ya miezi tisa ya kuomba na kusali na pia uvumilivu mkali, jaribio la mauaji yaliyogonga vichwa vya habari sana ya mwanabiashara Monica Kimani huanza asubuhi hii katika Mahakama Kuu Nairobi.
Wakenya wapo macho kujua haswa ni nini kilifanyika katika uhusiano wa mtangazaji shupavu na mchumba wake Jowie.
Je, kunani?
Mwanahabari Jacque Maribe na mpenzi wake wa zamani Joseph Irungu leo wataonekana mahakamani ili kusikia jaribio la kesi dhidi yao ya mauaji ya Monica Kimani.
Itakumbukwa kuwa Monica Kimani aliuawa katika ghorofa yake ya bustani ya Lamuria usiku wa Septemba 19, 2018 baada ya kufika kutoka Juba, Kusini mwa Sudan, ambapo aliendesha biashara ya familia yake na alikuwa akienda Dubai kwenda kukutana na mpenzi wake.
Matarajio ya kesi hiyo haijabainika lakini iwapo Jowie na Maribe watapatikana kuwa na makosa, wataweza kupata mashtaka ya kifo.
Kanuni ya Adhabu Sehemu ya 204 inasema kwamba mtu yeyote anayepatikana na hatia ya mauaji, wizi wa kimabavu, uhalifu na makosa mengine makubwa atanyongwa.
Lakini je, mwendesha mashtaka Catherine Mwaniki atamshawishi Jaji Philip Wakiaga kwamba wawili hao walihusika kwenye maandalizi ya mauaji?
Baadhi ya washahidi ambao watatoa ushahidi wao ni pamoja na Brian Kasaine na rafiki wa karibu wa Jowie Jennings Orlando.
Orlando na Kasaine walikuwa wameachiliwa baada ya kujitolea kusaidia serikali kwa uchunguzi. Bunduki la Kasaine pia inasemekane Jowi alilitumia kujipiga risasi.