Rais Uhuru Kenyatta siku ya Ijumaa alisifu mradi wa stesheni za Huduma ambazo zilizinduliwa na Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru wakati alikuwa waziri wa ugatuzi
katika Siku ya Huduma ya Umma ya Afrika iliyofanyika KICC, alisema kuwa mradi huo, ambao umemtambulisha Waiguru kimataifa, umetumikia Wakenya milioni 24 na kuokoa nchi Ksh74 bilioni.
“Vituo hivi hutoa huduma zaidi ya 104 tofauti na ya kuridhisha wateja kwa asilimia 95, ” rais alibainisha.
Ofisi za Huduma ziliwekwa katika kila kanti ili uhakikisha utoaji wa huduma umefikia kila mwanachi na kwa wakati unaofaa.
Aliwakumbusha watumishi wa umma waliohudhuria haja ya kuweka kipau mbele utoaji wa huduma kwa wananchi.
“Kazi hii kuu inaomba kujitolea; maono wazi na thabiti; uongozi wa ujasiri; na, juu ya yote mengine, kukuza uaminifu na utamaduni wa kutia bidii, “Rais Kenyatta aliongezea.
Baadhi ya wajumbe wa ngazi ya juu ambao walihudhuria mkutano huo walikuwa Waziri na wawakilishi kutoka nchi 35 za Umoja wa Afrika.