Mwanahabari mashuhuri Jeff Koinange amegonga vichwa vya habari baada ya kutaja neno lililoonekana kama ‘mwiko’ na wengi akisoma habari.
Mwanahabari huyo wa televisheni ya Citizen alikuwa anasoma taarifa ya mapacha wawili wa Kakamega ambao walijaajaa kwenye mitandao ya kijamii mwezi iliyopita.
Chembechembe za DNA zilitoka wiki iliyopita na ikafahamika kwamba Sharon na Melvin ni mapacha kwa asilimia mia.
Akitangaza na mwenziwe Victoria Rubadiri, Jeff Koinange alimalizia taarifa yake akisema kuwa watatu hao, Melvin, Sharon na Melon watakuwa na ‘threesome’ ya kufana.
Kwenye kamusi ya Oxford, ‘Threesome’ ama ‘utatu’ ni kitu chochote kile ambacho kinafanywa na watu watatu kama vile kutembea, kukula na hata pia kusoma.
Jeff Koinange must have passed through Koinange Street before reading news, Citizen TV what's an "awesome threesome"?
News in Kenya has become explicit content. Rubadiri couldn't stomach Jeff comments pole. 😂😂😂 pic.twitter.com/VrupFoIOkG
— Cyprian, Is Nyakundi (@CisNyakundi) June 17, 2019
Hata hivyo, kwa maana nyingine ambayo imevuma sana mtandaoni ni kushiriki ngono mkiwa watu watatu. Mashabiki waliotazama taarifa hiyo wanasema kwamba neno hilo halikufaa kuongelewa televisheni.
https://twitter.com/MutuNne/status/1140565572016582656
So when three people live happily in one house it's called 'threesome'? 🤔 Thank you Jeff Koinange for this.. I always thought that threesome meant something else. So did Rubadiri 😂
— Otieno Dave (@MseriousMcee) June 17, 2019