DIAMOND PLATNUMZ & MORGAN HERITAGE KUUJAZA UWANJA WA MPIRA KENYA.

Msanii wa Bongo Fleva Naseeb Abdul ama Diamond Platnumz anatarajiwa kupiga  show jijini Nairobi katika uwanja wa mpira wa Moi Kasarani siku ya tarehe 8 ya mwezi huu katika tamasha la ‘Tomorrow’s Leaders Festival’lilioandaliwa na kundi la muziki la Morgan Heritage la nchini Jamaica.

kupitia akaunti yake ya instagram Diamond Platnumz alithibitisha juu ya kushiriki tamasha hilo kwa kupost kipande cha video kwaajili ya promo.

 

View this post on Instagram

 

NAIROBI!!! NAIROBI!!!! KENYA!!! SEE YOU AT KASARANI STADIUM NEXT WEEK ON THE 8TH JUNE KWA TOMORROW’s LEASER’s FESTIVAL ya @morganheritage ….!!! #SIMBAinNAIROBI #SIMBAinKENYA

‘Tomorrow’s Leaders Festival’ ni tamasha la hisani liliLondaliwa na kundi la Morgan Heritage ili kuchangisha fedha za kuendeleza program ya Uongozi iliyoasisiwa na kundi hilo barani Afrika na nchini Jamaica.

Diamond kwa sasa anafanya vizuri na hit song ya Inama aliyomshirikisha Fally Ipupa toka nchini Congo , Diamond Platnumz pia ana collabo lililofanya vizuri na kundi la Morgan Heritage liitwalo haleluyah  nae alishirikishwa pia kwenye wimbo wa ‘Africa Jamaica’ wa kundi hilo.

Mbali na Diamond Platnumz wasanii wengine ni mwanadada Alain kutoka Jamaica,Wyre toka kenya, Yemi Alade from Naija, Jose Chameleone from Uganda na wenyewe Morgan Hertage na wasanii wengine kibao.

 

View this post on Instagram

 

#Nairobi, #Kenya it’s time for us to come home! Join us on June 8th as we start a movement to save a generation. Get your early bird tickets now! Tickets available at Link in Bio or MPESA Paybill 951802 🇰🇪🇯🇲 . #MorganHeritage #TLF2019 @2morrowleader #TomorrowsLeadersFestival #LOYALTY #AfricaJamaica #PayAttention #Global @alainesinga @diamondplatnumz @yemialade @stonebwoyb @jchameleon @iamjemere @wyredalovechild @juacaligenge @krissdarlin @ctbcmusicgroup @morganheritageloyalroyalsfans @kicproductions1

KUHUSU MOI KASARANI STADIUM

Unajulikana kama Uwanja wa Kimataifa wa Michezo wa Moi na shughuli mbalimbali hufanyika kwenye uwanja huu ambao hubeba takribani watu 60000 uko nje kidogo ya jiji la  NairobiKenya.

Ulijengwa mwaka 1987 na ulifadhiliwa na serikali ya China kwa ajili ya All-Africa Game iliyofanyika mjini Nairobi. Unatumika kwa sasa haswa kwa mechi za kandandaTimu ya Kitaifa ya Kenya huchezea mechi zake nyingi za nyumbani hapa. Kando na uga wa kandanda, kuna pia ukumbi unaobeba watu 5,000 wa Gymnasium na ukumbi wa kuogelea kama sehemu ya Uwanja wa Kimataifa wa Michezo wa Moi.

Katika nyanja za burudani ya muziki uwanja huu unahistoria ya kufanyika  Sherehe za mwaka wa 2009 za MTV Africa Music Awards zilizoandaliwa na kituo cha luninga cha MTV.

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *